Tuesday, November 15, 2016

NAMNA YA KUTENGENEZA MAANDAZI



Chukua Amira ya chenga gram 11



Chumvi nusu kijiko kidogo cha chai


Sukari gram 250


Unga wa ngano kilo moja

Maji ya uvugu vugu nusu lita



Mafuta ya kupikia lita 2 na nusu

Weka pakiti ndogo ya amira yenye ujazo wa gramu 11 yoote kwenye unga wako wa kilo moja



Kisha weka chumvi nusu kijiko kidogo cha chai chumvi hii husaidia kupunguza mafuta ndai yaa andazi baada ya kuiva andazi lako litakua halina mafuta safi na salama kwa mlaji

Weka sukari gram 250 katika unga wako


Baada ya hapo weka mafuta ya moto ujazo wa kikombe kidogo cha chai au gr 250
 changanya vizuri mafuta bado yakiwa yamoto


Kisha weka maji ya uvuguvugu ili kuuwa ngano nakufanya amira kuweza kumuka haraka



Kanda mchanganyiko wako safi kwa kutumia nguvu na umakini mpaka mchanganyiko wako uwe laini


Mchangyanyiko wako kama uko bado ni teketeke na ulizidisha maji kidogo weka unga kiasi kisha endelea kukanda mpakja uwe mkavu na laini

Hapa safi sasa


 Shepu vizuri tayari kwa maandalizi ya kusukuma na kukata 



Sukuma unga wako mpaka saizi ya unmene halisi wa andazi lako utakavyopenda liwe

Kisha tumia kitu chechote kile kukatia kwa umbo lolote lile utakalo lipenda



Yaache kwa muda wa dakika 10 baada ya kuyakata yaumuke kisha itakua tayari kwa kuyachoma


Baada ya kukata maumbo mazuri ya duara unga unaobakia unaweza viringisha maumbo tofauti kama uonavyo katika picha pia unaweza tengeneza hata herufi

 Pasaha mafuta yako katika moto wa wastani yasiwe na moto mkali utapelekea maandazi yako kuungua kisha yaweke katika moto na geuza kila mara ili yasivimbe upande mmoja na ikawa vigumu kuyageuza




Hili ni anfazi lako safi limeshaiva na halina mafuta ndani na safi kabisa

15 comments: