Tuesday, November 15, 2016

Mapishi ya Chapati za maji



Mahitaji

  • Unga wa ngano (plain flour) ( 1/4 kilo)
  • Yai (egg 1)
  • Sukari (sugar 1/4 kikombe cha chai)
  • Chumvi (salt 1/4 kijiko cha chai)
  • Hiliki (ground cardamon 1/4 kijiko cha chai)
  • Maji kiasi
  • Mafuta (vegetable oil)
Matayarisho
Tia unga kwenye bakuli, kisha weka sukari, chumvi, hiliki na maji kiasi. Kisha koroga mpaka mchanganyiko wako uwe mzito. Baada ya hapo tia yai na ukoroge tena. hakikisha mchanganyiko hauwi mzito sana au mwepesi sana.Baada ya hapo onja kama kila kitu kimekolea. Injika chuma cha kupikia chapati (fry-pan) jikoni  katika moto wa wastani. Baada ya hapo tia nusu kijiko cha chakula cha mafuta katika fry-pan na kisha yatandaze. Hakikisha chuma kinapata moto na weka upawa mmoja wa unga wa chapati na uutandaze mpaka uwe flat. Baada ya hapo subiri mpaka chapati ikauke juu na kisha igeuze upande wa pili tia mafuta kijiko 1 kikubwa cha chakula kwa upande wa chini na wa juu kisha uanze kuikandamiza kwa juu na kijiko ili iweze kuiva vizuri kwa chini. Ikisha kuwa ya rangi ya brown igeuze na upike upande wa pili kiasi kisha iipue na uiweke kwenye sahani yenye kitchen towel ili kukausha mafuta. Rudia hii process kwa unga wote uliobakia. Na chapati zitakuwa tayari

NAMNA YA KUTENGENEZA MAANDAZI



Chukua Amira ya chenga gram 11



Chumvi nusu kijiko kidogo cha chai


Sukari gram 250


Unga wa ngano kilo moja

Maji ya uvugu vugu nusu lita



Mafuta ya kupikia lita 2 na nusu

Weka pakiti ndogo ya amira yenye ujazo wa gramu 11 yoote kwenye unga wako wa kilo moja



Kisha weka chumvi nusu kijiko kidogo cha chai chumvi hii husaidia kupunguza mafuta ndai yaa andazi baada ya kuiva andazi lako litakua halina mafuta safi na salama kwa mlaji

Weka sukari gram 250 katika unga wako


Baada ya hapo weka mafuta ya moto ujazo wa kikombe kidogo cha chai au gr 250
 changanya vizuri mafuta bado yakiwa yamoto


Kisha weka maji ya uvuguvugu ili kuuwa ngano nakufanya amira kuweza kumuka haraka



Kanda mchanganyiko wako safi kwa kutumia nguvu na umakini mpaka mchanganyiko wako uwe laini


Mchangyanyiko wako kama uko bado ni teketeke na ulizidisha maji kidogo weka unga kiasi kisha endelea kukanda mpakja uwe mkavu na laini

Hapa safi sasa


 Shepu vizuri tayari kwa maandalizi ya kusukuma na kukata 



Sukuma unga wako mpaka saizi ya unmene halisi wa andazi lako utakavyopenda liwe

Kisha tumia kitu chechote kile kukatia kwa umbo lolote lile utakalo lipenda



Yaache kwa muda wa dakika 10 baada ya kuyakata yaumuke kisha itakua tayari kwa kuyachoma


Baada ya kukata maumbo mazuri ya duara unga unaobakia unaweza viringisha maumbo tofauti kama uonavyo katika picha pia unaweza tengeneza hata herufi

 Pasaha mafuta yako katika moto wa wastani yasiwe na moto mkali utapelekea maandazi yako kuungua kisha yaweke katika moto na geuza kila mara ili yasivimbe upande mmoja na ikawa vigumu kuyageuza




Hili ni anfazi lako safi limeshaiva na halina mafuta ndani na safi kabisa